Search
Close this search box.

Maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Saratani Duniani – Dar es Salaam

Dar es salaam, Tanzania

Leo tarehe 4 Februari 2024, katika viwanja vya Mbagala Zakhiem, yalifanyika maadhimisho ya kilele cha Siku ya Saratani Duniani yakiongozwa na Mgeni rasmi, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dkt. Rashid Mfaume.

Washiriki na Wadau

Maadhimisho haya yaliratibiwa na kushirikisha wadau mbalimbali wa afya wakiwemo:

  • NACOPHA
  • Taasisi ya Saratani Ocean Road
  • TAMISEMI
  • WHO
  • TAS
  • Mashujaa Cancer Foundation

Yote haya yalifanyika chini ya usimamizi wa Wizara ya Afya kwa kauli mbiu isemayo, “Saratani Inazuilika Huduma Sawa kwa Wote.”

Shughuli za Kiafya

Katika maadhimisho haya, kulikuwa na shughuli mbalimbali za kiafya zikiwemo:

  • Upimaji na uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi, tezi dume, na saratani ya matiti
  • Utoaji wa damu salama
  • Upimaji wa shinikizo la damu na kisukari
  • Huduma nyingine nyingi za kiafya

Uzinduzi wa Afya Game

Aidha, kulikuwa na uzinduzi wa Afya Game, mchezo wa bahati unaolenga kuchangia huduma za afya kwa wagonjwa wa saratani huku ukitoa nafasi za kushindia zawadi mbalimbali. Wageni mbalimbali walichangia huduma hii kwa moyo mkunjufu.

Hotuba ya Mgeni Rasmi

Mgeni rasmi, Dkt. Rashid Mfaume, alitambua kazi kubwa inayofanywa na NACOPHA katika mwitikio wa UKIMWI na mchango mkubwa wa WAVIU katika ufuasi mzuri wa dawa. Pia, alitambua ushiriki wa NACOPHA katika uzinduzi wa mpango jumishi wa wahudumu wa afya ngazi ya jamii.


Kwa habari zaidi na updates, tafadhali tembelea tovuti yetu au fuatilia mitandao yetu ya kijamii.

SikuYaSaratani #NACOPHA #AfyaKwaWote #SarataniInazuilika #AfyaGame

Picha za Matukio

Share the Post:

Get Involved

Make a Difference with NACOPHA

Your support helps us achieve our goals. Whether you volunteer your time, donate resources, or partner with us, your involvement makes a significant impact in the lives of people living with HIV/AIDS in Tanzania.

  • Join us in the fight againt HIV.
  • Let’s work together to provide support for those in need.
  • Donate to our cause