Search
Close this search box.

Ziara ya Kamati ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI Katika Konga ya Singida Vijijini

Singida, Tanzania

Kufuatia ziara ya Kamati ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika mikoa ya Singida, Mwanza na Tabora, Kamati hiyo imezuria Konga ya Halmashauri ya Singida Vijijini na kujionea shughuli za mwitikio wa UKIMWI zinazotekelezwa na Konga hiyo.

Katika ziara hiyo, Konga ya Singida Vijijini ilionesha shughuli za kiuchumi za vikundi na pia kutoa maelezo ya utoaji huduma za UKIMWI kwa jamii.

Vikundi Vilivyoshiriki

Vikundi vilivyoshiriki katika ziara hiyo ni pamoja na:

  • WAVUMA Group
  • WAVIU Group
  • Muungano Group
  • Wema Group
  • Majaaliwa Group

Wanachama wa vikundi hivyo walikiri kwa Kamati ya Bunge ya Afya kuwa shughuli hizi zimewasaidia kudumu katika dawa za kufubaza VVU, kutokuwa tegemezi, na pia kuwa karibu na fursa za uwezeshwaji zilizopo.

Ufafanuzi wa Muundo wa NACOPHA

Akitoa ufafanuzi wa muundo wa NACOPHA, Bi. Victoria Huburya alipongeza jitihada za Serikali katika kutoa huduma za UKIMWI nchini na hususan huduma za tiba na matunzo. Pia alisisitiza kuwa kupitia vikundi vya WAVIU, unyanyapaa binafsi umepungua. Mradi wa Hebu Tuyajenge umeongeza hamasa kwa WAVIU kutumia huduma za UKIMWI zilizopo.

Aidha, Bi. Victoria alishukuru ushirikiano wa halmashauri zote nchini kwa Konga zote za NACOPHA na pia kuomba ushirikiano zaidi kwa Konga na wadau wengine kwa kuwa shughuli za mwitikio wa UKIMWI ni endelevu.

Maneno ya Mh. Ummy Ndaliananga (Mb)

Akizungumza na WAVIU, Mh. Ummy Ndaliananga (Mb) alisisitiza umuhimu wa kuwafikia wananchi kwa huduma bora za UKIMWI na kuendelea kupambana na unyanyapaa. Ziara hii ni mara ya kwanza kwa Konga ya Singida Vijijini kutembelewa na Kamati hiyo.


Kwa habari zaidi kuhusu ziara na juhudi zetu za kupambana na UKIMWI, tafadhali tembelea tovuti yetu hapa au fuatilia mitandao yetu ya kijamii.

Picha za Matukio

Share the Post:

Get Involved

Make a Difference with NACOPHA

Your support helps us achieve our goals. Whether you volunteer your time, donate resources, or partner with us, your involvement makes a significant impact in the lives of people living with HIV/AIDS in Tanzania.

  • Join us in the fight againt HIV.
  • Let’s work together to provide support for those in need.
  • Donate to our cause